Afrika kupata chanjo karibu milioni 1 ya mpox: ripoti

0

Jumuiya ya afya ya Umoja wa Afrika imetangaza kuwa inakaribia kupata dozi karibu milioni moja za chanjo ya mpox, huku ikihimiza watengenezaji wa chanjo kushirikiana katika teknolojia ya utengenezaji ili kupambana na ugonjwa huu.

Mkurugenzi Mkuu wa Vituo vya Kudhibiti Magonjwa Afrika (Africa CDC), Jean Kaseya, alifafanua kwenye mkutano wa WHO uliofanyika Congo-Brazzaville kwamba Afrika inakaribia kupata dozi hizi. Nchi kadhaa zimeahidi kutoa chanjo kwa nchi zilizoathirika, huku Hispania pekee ikiwa na ahadi ya kutoa dozi 500,000.

Kaseya alifichua kuwa dozi 215,000 tayari zimepatikana kutoka kwa mtengenezaji kutoka Denmark, Bavarian Nordic, lakini alisisitiza umuhimu wa kushirikiana katika teknolojia ili chanjo hizo ziweze kutengenezwa barani Afrika. Aliongeza kuwa anaamini chanjo ya mpox itaanza kutengenezwa Afrika hivi karibuni.

Kaseya alibainisha kuwa visa 22,863 vinavyohusishwaa na vifo 622 vilivyotokea hadi Agosti 27 vinahusishwa na aina mbalimbali za virusi vya mpox barani Afrika. Hata hivyo, alionyesha kuwa hakupenda kutoa maelezo ya kina kuhusu visa vilivyothibitishwa kwa sababu baadhi ya nchi zina kiwango cha kupima chini ya asilimia 30 na zinakutana na changamoto kadhaa za ubora na usafirishaji.

Mpox, ambapo awali ulijukana kama Monkeypox, ni ugonjwa wa virusi unaotokana na maambukizi kutoka kwa wanyama hadi kwa wanadamu na unaweza pia kuenea kutoka kwa binadamu hadi kwa binadamu.

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambako aina hiyo mpya ya virusi iligunduliwa kwa mara ya kwanza, imeathirika sana na janga hili, ikiwa na asilimia 90 ya visa vilivyoripotiwa mwaka huu. Huku nchi nyingine zilizohusika ni Burundi, Rwanda, Kenya, na Uganda.

Kwa mujibu wa WHO, Afrika iliripoti visa 5,281 vya mpox kuanzia mwanzo wa mwaka hadi Agosti 25.

0 0 votes
Article Rating
Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x